Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wachimbaji wadogo wa madini watengewa eneo maalum


a.Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud (kushoto) akitoa taarifa yake.Kuliwa kwakeni ni Kaimu Mkurugeniz wa Idara ya Habari Maelezo,Zamaradi Kawawa.
Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud, (kushoto) akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo pichani).  Kulia kwake ni Kaimu Mkurugeniz wa Idara ya Habari Maelezo,  Zamaradi Kawawa.   
b.Waandishi wa habari wakichukua taarifa hiyo.
Waandishi wa habari wakifuatilia taarifa hiyo.
c.Badra (kushoto) akiendelea kutoa ufafanuzi wa jambo.
Badra (kushoto) akiendelea kutoa ufafanuzi.
SERIKALI kupitia wizara yake ya Nishati na Madini imesema imetengea maeneo maalumu  wachimbaji madini wadogo nchini jumla ya hekari 197,432.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud,  amesema lengo la kutenga maeneo hayo ni kuendeleza uchimbaji madini mdogo ili kuwanufaisha wachimbaji .
Amesema wizara imekuwa ikitenga maeneo maalumu au tengefu kwa ajili ya wachimbaji madini wadogo pekee ambao ni Watanzania tu , zoezi hilo hufanywa kwa mujibu wa sheria ya madini ya mwaka2010 kifungu cha 16 kinachompa mamlaka Waziri wa Nishati na Madini kuhakikisha anatenga eneo lililo wazi  na lenye madini kwa ajili ya wachimbaji wadogo.
Badra amesema, mara tu baada ya waziri kumaliza kutenga eneo hilo kinachofuata ni utaratibu wa kugawa  hilo eneo kwa kwa kufuata taratibu za  kisheria.
Aidha amebainisha maeneo 34 ya sehemu mbalimbali za hapa nchini yaliyotengwa yenye ukubwa wa hekta197,432 ambayo miongoni mwa mwake ni, Mererani Block 1-V (Manyara), Kilindi (Tanga), Maganzo (Shinyanga), Mihama (Mwanza), Winza(Dodoma), Kalela (Kigoma) na maeneo mengine aliyoyataja.
Wakati huohuo alisema serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia imetenga kiasi cha Dola za Marekani milioni 3.4 kwa miaka mitatu kuanzia mwaka huu wa fedha 2015/16 kwa ajili ya kuwawezesha wachimbaji madini wadogo kwa kuwapatia ruzuku ikiwa ni awamu ya tatu ili waweze kuchimba kwa mfumo wa kisasa na kujiongezea vipato vyao pamoja na pato la taifa.
Katika hatua nyingine alisema utaratibu wa wachimbaji wadogo kupatiwa ruzuku ni lazima kwanza wawe na leseni ya uchimbaji, kujaza fomu za kuomba ruzuku na kutoa ushirikiano kwa maofisa madini wa kanda na maofisa wa madini wakazi husika eneo hilo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top