Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

January Makamba "Amwanika" Rais Magufuli



MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, January Makamba amesema kasi ya utendaji inayooneshwa na Rais John Magufuli na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, imekipa uhai mpya chama chao na kwamba wanaCCM sasa wanatakiwa kutembea kifua mbele.

Akizungumza jana na mwandishi wetu Dar es Salaam, January alisema wakati wa kampeni CCM iliahidi itawaletea Watanzania mabadiliko na jambo hilo ndilo hasa linalofanywa na Magufuli na Majaliwa.

“WanaCCM sasa wanatakiwa kutembea kifua mbele na kuwapongeza Magufuli na Majaliwa kwa kutoa matamko ya kuwaunga mkono kwa hatua wanazochukua. Wakati wa kampeni tuliahidi mabadiliko ya kweli. Na sasa tunaanza kuyaona,” alisema January na kuongeza:

“Tusikae kimya. Hii ni vita kali na naamini Watanzania wote wanamuunga mkono, lakini kwa kuwa anatekeleza ahadi ya CCM sisi tunapaswa kuwa mstari wa mbele kwa kumuunga mkono kwa maneno na matendo.

“Tulipigana kufa na kupona ili tushinde na baadhi yetu tunaendelea kupokea vitisho na matusi kwa sababu ya kampeni kwa vile kwa wapinzani ushindani haujamalizika baada ya kumalizika kwa kampeni. "  
Mbunge huyo wa Bumbuli mkoani Tanga na Naibu Waziri katika Serikali ya Awamu ya Nne, alisema kama mwana CCM na MNEC anajisikia fahari kwa vitendo vinavyofanywa na Magufuli kwa vile vimekipa chama pumzi na uhai mpya, akikumbusha maneno yaliyokuwa yakitumika na wapinzani kwamba chama hicho sasa kimeishiwa pumzi.

“Lazima CCM ihakikishe Magufuli na Majaliwa wanafanikiwa katika uongozi wao. Hapo ndiyo nguvu iliyotumika katika kampeni itakuwa na maana. Kazi anayofanya Rais inakiletea chama pumzi na uhai mpya.

“Kwa mwendo huu, hakutakuwa na kazi ngumu katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kama ilivyokuwa mwaka huu. Inawezekana wapo wanaCCM watakaoguswa na utendaji huu wa Rais, lakini hiyo ni gharama ndogo sana ya kulipa kwenye kuitafuta Tanzania ambayo kila mwananchi anaililia,” alisema.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top