Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Jaji Utamwa, Fungamtama Uso kwa Uso na David Kafulila Katika Kesi ya Ubunge



KESI ya matokeo ya ubunge katika Jimbo la Kigoma Kusini iliyofunguliwa na David Kafulila, inamkutanisha uso kwa uso na Jaji John Utamwa lakini pia wakili Kennedy Fungamtama..

Fungamtama alikuwa wakili wa Kampuni ya Dowans katika kesi dhidi ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco) wakati Jaji Utamwa ndiye aliyetoa hukumu ‘tata’ ya kesi ya kampuni ya kufua umeme wa dharura (IPTL) mwaka 2013 iliyozaa sakata la ufisadi kwenye Akaunti Escrow.

Kwenye kesi ya Dowans dhidi ya serikali (Tanesco), Wakili Fungamtama akiitetea Dowans alishinda wakati katika kesi ya IPTL, Jaji Utamwa alitoa hukumu inayotajwa kuwa chanzo cha sakata la uchotwaji wa zaidi ya Sh. 306 bilioni kwenye Akaunti ya Esrcow bungeni mwaka 2014.

Hatua ya kuchotwa kwa fedha hizo ndiyo iliyomuibua Kafulila ambapo alidai kuwepo kwa ufisadi katika uchotaji huo.

Katika kesi ya uchaguzi ya Kafulila, wakili Fungamtama amesimama kumtetea mbunge wa jimbo hilo, Hasna Mwilima aliyetangazwa kushindwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambapo Jaji Utamwa ndiye aliyepangiwa kusikiliza kesi hiyo.

Kwenye kesi hiyo Kafulila anayetetewa na wakili Daniel Lunyemela ambapo anaiomba Mahakama Kuu Kanda ya Tabora imtangaze kuwa mshindi halali wa uchaguzi huo kama ambavyo kura za jumla katika fomu za matokeo ya vituo vyote 382 zinaonesha tofauti na matokeo yaliyotangazwa.

Wakili Fungamtama anayekumbukwa kama wakili wa kampuni ya Dowans katika kesi ya madai Na.8/2011 iliyofunguliwa na Tanesco kupinga kusajiliwa katika Mahakama Kuu nchini hukumu ya kuilipa Dowans kiasi cha fedha zaidi ya bilioni 94 sasa anamkabili Kafulila ambaye ndiye mlalamikaji katika kesi hiyo.

Fungamtama pia anatajwa kama wakili ghali sana hapa nchini na duniani kutokana na gharama kubwa ambazo hutoza wateja wake wanaohitaji huduma ya kisheria huku akisifika pia kwa kumudu na kujua kucheza ‘siasa za kisheria’ katika kesi mbalimbali anazosimamia.

Hata hivyo Kafulila anaeleza kuwa kesi yake ipo ‘wazi’ kwa kuwa anavyo vielelezo vyote kutoka katika vituo 382 vya kupigia kura na kwamba atashinda.

Mwandishi wa habari hizi amemtafuta Kafulila ili kueleza mtazamo wake juu ya kesi hiyo kusikilizwa na Jaji John Utamwa lakini pia Mwilima kutetewa na Fungamtama, hata hivyo hakupatikana.

Kesi hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi namba 2/2015 katika Mahakamu Kuu ya Tabora inaendelea leo jumatatu Novemba 30 ambapo Jaji Utamwa atasikiliza ombi lililowasilishwa na Kafulia akitaka kupunguziwa malipo ya dhamana kwani anatakiwa kulipa dhamana ya Sh. 15milioni kutokana na kulalamikia washitakiwa watatu.

Washitakiwa hao watatu ni Hasna Sudi Mwilima (CCM) ambaye ni mbunge, msimamizi wa uchaguzi huo Reuben Mfune pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Geoge Masaju.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top