Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ZARI NDANI YA BIFU ZITO NA MAMA DIAMOND .... DIAMOND ACHANGANYIKIWA


DSC_5716Zarinah Hassan ‘Zari’

Waandishi wetu

NI vita! Baada ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwenda nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ kumwangukia mzazi mwenzake, Zarinah Hassan ‘Zari’ kufuatia kuwepo kwa figisufigisu kati yao huku mama wa msanii huyo, Sanura Kassim ‘Sandra’ akihusishwa, mazito yameibuka.

TUJIUNGE NA CHANZO
Habari kutoka chanzo cha ndani ya familia ya Diamond zinamwagika kwamba, Zari amekubali kuja Bongo lakini akatoa sharti: “Nakuja Bongo, Desemba 8, lakini mama (mama mkwe) aondoke pale nyumbani (Tegeta-Madale, Dar).”

ZARI ATIA NGUMU, AKUBALI
Chanzo hicho kilimwaga ‘ubuyu’ kwamba, awali Zari alimtilia ngumu Diamond lakini baadaye alikubali kurejesha amani kama ilivyokuwa zamani hivyo watakuja wote Bongo baada ya kujiachia vya kutoka huko Sauzi nyumbani kwa mwanadada huyo.

mama-diamondMama Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’

DIAMOND KICHEKO SAUZI
Kuhusu kuweka mambo sawa na kuwa atarejea Bongo na Zari na mtoto wao, Latiffah ‘Tiffah’, Diamond alilidokeza gazeti hili kwamba, sasa ni ‘full’ kicheko na anamshukuru Mungu kwa kufanikisha kufanya mambo kuwa kama mwanzoni.

Alitamba kuwa atatinga Bongo wiki hii au mapema wiki ijayo akiambatana na familia yake kwani kwa sasa wapo poa na hakuna manenomaneno tena.

“Nakuja na familia yangu. Kwa sasa tupo poa sana na maisha yanaendelea. Kiukweli huku South (Sauzi) tuna amani sana,” Diamond aliliambia gazeti hili wikiendi iliyopita.

TURUDI KWA CHANZO BONGO
Ilidaiwa kwamba, baada ya mama Diamond kusikia kuwa, mwanaye atarejea Bongo, Desemba 8, mwaka huu akiambatana na Zari alianza kuhaha kwa vile alishamtolea maneno makali akidai kuwa, mkwewe huyo alikuwa analeta uzungu kwenye familia yake.

“Unaambiwa ndugu wanapomuonesha mama Diamond picha za Zari akijiachia na Diamond na mtoto wao, Tiffah, anaamini kweli anaweza kuja Bongo jambo ambalo hataki kulisikia,” kilisema chanzo hicho.

10843996_788400007864260_370710352_nDiamond na Zari

MAMA DIAMOND KAMA MAGUFULI
Kufuatia hali hiyo ilitonywa kuwa, mama Diamond alifunguka kimipasho:
“Hata kama akija ataondoka kurudi kwao kama alivyokuja kwani ‘Hapa Kazi Tu’ kama ilivyo kauli mbiu ya Rais John Pombe Magufuli.”

Ili kupata mzani wa habari hiyo, mmoja wa vijumbe wetu alimtafuta mama Diamond kwa njia ya simu ambapo aliwaka mara tu baada ya kuulizwa ishu hiyo.
Katika majibu yake ya hasira, mama Diamond alisema haogopi lolote na yupo tayari kwa lolote.

MSIKIE MWENYEWE
“Siogopi chochote Zari kurudi hapa, kama atakuja, atakuwa amekuja kama alivyokuja mwanzoni na ataondoka hivyohivyo kama alivyoondoka awali.
“Sasa kwani nina hofu gani wakati niko nyumbani kwangu hapa? Watu watuache na waache unafiki wa kufuatilia mambo ya watu,” alisema mama D kisha akakata simu.

TUJIKUMBUSHE
Mapema baada ya Zari kujifungua mtoto wa Diamond, kuliibuka maneno ya mama mkwe huyo kutoelewana na mama Tiffah ambapo mara tu baada ya sherehe ya 40 ya mtoto huyo, Zari alitimka Bongo kwa maelezo kwamba hatarejea lakini sasa anaweza kuja kupambana tena na mama mkwe wake anayeonekana bado ana jambo moyoni.

Imeandikwa na Gladness Mallya, Mayasa Mariwata na Musa Mateja
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top