Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli,akiwahutubia wananchi wa mji wa Mtwara
waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza kwenye mkutano wa kampeni
unaoendelea jioni hii katika uwanja wa Mashujaa.
Dkt John Magufuli
amesema kuwa iwapo atachaguliwa kuwa Rais katika uchaguzi mkuu mwaka huu
,Serikali yake itashusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa bati na saruji,amesema kuwa serikali yake inataka kurahisisha maisha ya
watanzania wote na hivyo atapunguza bei ya saruji na bati na hilo
litafanikiwa kwa kupunguza ushuru wa vifaa hivyo.
"Serikali ya Magufuli nataka iwe ya kurahisisha maisha ya
wananchi wake.Moja ya mambo ambayo ninedhamiria kuyafanya ni kupunguza
bei ya bati na saruji.Nataka kuona watu wanajenga nyumba nzuri na za
kisasa, hivyo lazima tushushe bei ya vifaa vya ujenzi,alisema
Dk.Magufuli.
Alisema anatambua kiu ya watanzania ni kutaka mabadiliko ya
maendeleo na kwamba Serikali yake itasimamia kuleta maendeleo ya
wananchi na kazi hiyo anaiweza na ndio maana anaomba urais. " Ndugu zangu watanzania serikali ya Magufuli inakuja
kuendelea pale ambapo awamu nyingine zimeishia.Tumetoka mbali ,tupo
mbali na tunakwenda mbali.Nataka tuwe na maendeleo makubwa na hilo
serikali yangu ndio kazi itakayofanya,"alisema Dk.Magufuli huku wananchu wakimshangilia kwa mayowe.
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi
Dkt John Pombe Magufuli,akiwahutubia wananchi wa mji wa Mtwara
waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza kwenye mkutano wa kampeni
unaoendelea jioni hii katika uwanja wa Mashujaa.
Wakazi
wa mji wa Mtwara wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa
hadhara wa kampeni za CCM,unaofanyika jioni ya leo kwenye uwanja wa
CCM,wakimsikiliza mgombea Urais wa chama hicho Dkt John Pombe Magufuli.
Mgombea
Ubunge wa jimbo la Mtwara mjini,Murji Hasnein Mohamed akiwasalimia
maelfu ya wananchi wa mji wa Mtwara waliofurika kwenye uwanja wa
Mashujaa katika mkutano wa kampeni za CCM,jioni ya leo ambapo Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John
Pombe Magufuli aliwahutubia wananchi hao .
Mgombea
Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akijiachia jukwaani pamoja na
wasanii wa kundi la Yamoto Band kwenye uwanja wa Mashujaa mkoani
Mtwara,ambapo Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao
waliofurika kwa wingi.
Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akijiachia jukwaani pamoja
na wasanii wa kundi la Yamoto Band kwenye uwanja wa Mashujaa mkoani
Mtwara,ambapo Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao
waliofurika kwa wingi.
Wakazi
wa mji wa Mtwara ambao wamejitokeza kwa wingi hivi sasa ndani ya uwanja
wa Mashujaa, mjini Mtwara kumsikiliza Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania,kupitia chama cha CCM,Dkt John Magufuli
Wananchi wakiwa wamekusanyika ndani ya uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara hivi sasa,kumsikiliza Dkt John Pombe Magufuli
Wananchi wakiwa wamekusanyika ndani ya uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara hivi sasa,kumsikiliza Dkt John Pombe Magufuli.
Msanii
wa Muziki wa Kizazi kimya,Ali Kiba akiimba mbele ya maelfu ya wananchi
wa Mtwara jioni ya leo kwenye mkutano wa Kampeni wa CCM,ambapo Dkt John
Pombe Magufuli anatarajia kuwahutubia.
PICHA NA MICHUZI JR-MTWARA
Post a Comment