Kupitia akaunti yake ya Instagram Lulu ameandika:
Nimeulizwa
na Wengi na pengine yanasemwa mengi kuhusu ni Chama kipi cha Siasa nina
support Kama ilivyoonekana Kwa Wasanii Wenzangu wengine..! Kwa kifupi
nitajaribu kufafanua machache Kwa huu uwezo mdogo wa kufikiri
nilijaaliwa na Mwenyezi Mungu..! Kwanza,kila binadamu/mwananchi ana
uhuru wa kuchagua na ku support anachokipenda…kwahyo sitangaa wala
kuchukia Flani ku support upande flani
Pili,Mimi
Kama mm(binafsi)hii ni Mara yangu ya kwanza kupiga kura kwahyo nimeamua
kuitumia Kwa busara na kuifanya iwe na kwanza isiyo na majuto Kwa
kutofuata mkumbo wowote wa ndugu,jamaa,marafiki au watu
walionizunguka..! Tatu,Nimependa kuitumia NAFASI hii zaidi Kwa UHUSIKA
wa ELIZABETH na sio LULU nikimaanisha ikiwa kila kura ya mwananchi wa
wakawaida ni ya siri na kuuridhisha moyo wake basi na mm nitakuwa
mwananchi wa kawaida kbsa katika hili..! Nne,natoa pongezi Kwa wasanii
wenzangu waloweza kushiriki Kwa namna moja au nyingine ktk ku support
upande mmoja au mwingine kwani wameonyesha ujasiri na mapenzi ya kweli
kwa vyama wanavyo support ila tu mabishano ya hoja ni mazuri zaidi na
yanaweza kuepusha ugomvi au kuvunja mahusiano yetu ambayo yalikuwepo
kabla ya uchaguzi na yatatakiwa kuendelea kuwepo baada ya uchaguzi..!
tano,nawatakia kila la kheri wagombea wote na natumaini uchaguzi utakuwa
wa sawa na haki..!
Post a Comment