Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Lowassa kupitia upya mikataba

Pg 1 lowassas

MAELFU ya wakazi wa mji wa Songea mkoani Ruvuma, jana walifurika katika uwanja wa Matalawe kuhudhuria mkutano wa kampeni wa mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) chini ya mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa.

Hali hiyo ilitokea mjini Songea jana jioni wakati Lowassa alipowasili akitokea Mkoa wa Njombe alikohutubia mikutano miwili ya hadhara juzi katika miji ya Makambako na Njombe.

Wakati wa mapokezi ya mgombea huyo mjini hapa, walikuwapo mamia ya vijana, akina mama, wazee na watoto ambapo walijipanga barabarani wakimsubiri awasili uwanjani hapo.

Mbali na maelfu ya wananchi waliokuwa barabarani, idadi kubwa ilikuwa uwanjani hapo huku kila mmoja akiwa na hamu ya kumwona mgombea huyo. Kutokana na hali hiyo, shughuli za kijamii kama maduka, baa na masoko, zilisimama kwa muda kwa kuwa wananchi wengi walikuwa wakimpokea Lowassa.

Wakati hayo yakiendelea, makundi ya vijana walikuwa wamepanda katika miti inayozunguka uwanja huo ulio jirani na shule za msingi za Matalawe na Mnazi Mmoja. Kutokana na wingi wa watu, baadhi ya vijana walilazimika kupanda katika moja ya madarasa ya jengo la Shule ya Msingi Mwembechai ambapo paa la jengo hilo lilinusurika kuporomoka baada ya kuzidiwa na uzito.

Akihutubia mkutano huo, Lowassa aliahidi kulijenga paa hilo baada ya kugundua uwepo wa tatizo hilo. Pamoja na hayo, alisema atakapoingia madarakani, ataiangalia mikataba yote ya madini ili kuona inavyowanufaisha Watanzania.

“Hata wakubwa huko walielewe hili, simaanishi kwamba nawatisha wawekezaji, bali nayasema haya kwa sababu hatuwezi kuwa na madini na gesi ya kuinufaisha dunia wakati Watanzania hawana ajira. “Hata deni la Taifa nitaliangalia ili tuone lilivyopatikana na jinsi lilivyotumika.

Hata kile kiwanda chenu cha tumbaku, nitakifufua ikiwa ni pamoja na kuwaletea umeme wa uhakika hapa Songea,” alisema. Awali akihutubia wananchi wa Jimbo la Madaba mkoani hapa, Lowassa aliwataka wanaomkosoa kuhusu utendaji wake, wajibu hoja badala ya kuongea maneno yasiyokuwa na msingi.

“Hao wenzetu wasipige kelele, wajibu hoja kwa sababu mimi tatizo langu ni umasikini wa Watanzania. Kama wana njia mbadala ya kuondoa umasikini waseme, wasipige kelele tu,” alisema Lowassa.

Akizungumzia kilimo, alisema atakapofanikiwa kuingia madarakani, pamoja na kuahidi kufuta kodi zote katika sekta hiyo, Serikali yake haitawakopa wakulima na kwamba ikitokea wakiwakopa, watakapolipwa watalipwa na fidia kama sehemu ya kuwainua.

Kuhusu kero ya umeme ambayo imekuwa ikiwasumbua wananchi wa Ruvuma kwa muda mrefu, alisema atakapoingia madarakani atapeleka umeme katika Jimbo la Madimba.

SUMAYE Naye Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, alisema mwaka huu ndiyo mwaka wa kuiondoa CCM madarakani kwa kuwa matatizo waliyonayo Watanzania hayawezi kuondoka kama chama hicho kitaendelea kutawala. “Huu ndiyo mwaka wetu wa kufanya mabadiliko, na nawaambia kama msipokubali kuiondoa CCM madarakani kwa kuipigia kura Chadema na wagombea wa Ukawa, maisha yenu yataendelea kuwa mabaya.

“Haiwezekani nchi hii ikaendelea kuwa masikini, nawaambia umasikini tulionao ni wa kujitakia. “Msimchague Magufuli kwa sababu hana nia njema na Watanzania, na ndiyo maana hata alipokuja hapa juzi akielekea Ludewa, barabara hii ilimwagiwa maji ili asipate vumbi,” alisema Sumaye.

Pia, alisema viongozi wa CCM wanaomchafua Lowassa hawana hoja za msingi bali wanafanya hivyo kwa kuwa wanamwogopa. Sumaye aliwataka Watanzania wasiogope kufanya mabadiliko ya uongozi kwani kitendo chake na Lowassa kuhamia Ukawa ni kielelezo cha kutaka kuimarisha demokrasia wakiwa nje ya CCM
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top