Mapenzi
ya mwimbaji wa R&B Juma Jux na Vanessa Mdee a.k.a Vee Money sasa
yamefikia kwenye ‘climax’. Licha ya kukiri hadharani kuhusu uhusiano wao
lakini sasa kila mmoja wao amekuwa tayari kuelezea jinsi anavyompenda
mwenzie hadharani ikiwa ni ishara ya kuwa mahaba yako kileleni.
Jux
katika kusheherekea siku yake ya kuzaliwa ambayo ilikuwa ni Sept 1,
aliamua kuifanya kuwa siku maalum kumuandikia barua ya mapenzi Vanessa,
lakini haikuwa barua ya kawaida kama tulivyozoea bali ni barua ya moyo
wake kumzungumzia jinsi alivyobadili maisha yake toka wamekuwa wapenzi.
“Tomorrow
is my birthday nitaifanya maalum kwa msichana aliye badilisha maisha
yangu. Nitaiweka wazi barua ya moyo wangu ambayo huwa naisoma kila siku
kwenye nafsi yangu.” Aliandika Jux Instagram siku moja kabla ya birthday yake.
Kupitia
kipindi cha Ala za Roho cha Clouds Fm, Jux akiwa na Vanessa walipata
nafasi ya kuzungumzia mengi kuhusu uhusiano wao, na ndipo Jux alipewa
nafasi na Diva kuisoma ile barua yake ya moyo kuhusu Vanessa.
Yafuatayo ni mambo sita ambayo Jux aliyasema kuhusu jinsi Vanessa alivyobadilisha maisha yake toka wawe couple.
1. Cha
kwanza Jux alisema kuwa toka amekuwa na Vanesa Mdee mwaka 1 na miezi 8
sasa hajawahi kumcheat na msichana mwingine yeyote.
“Vanessa
ni msichana wangu ambaye, huu ni ukweli naongea…ni mahusiano yangu
ambayo nimekuwa na Vanessa halafu sijawahi kuwa na msichana mwingine
yeyote, samahani kwa ma ex wangu nilikuwa nao lakini nilikuwa na maside
chicks..Ni msichana ambaye nimekuwa nae na sijawahi kuwa na mwanamke
mwingine yeyote kwa muda wa mwaka mmoja na miezi karibia nane.” – Jux
2.Kitu
cha pili Jux alisema kuwa Vanessa amekuwa msaada mkubwa sana kwenye
muziki wake kiasi ambacho hadi sasa kuna hatua kubwa ambayo ameipiga
kutokana na miongozo yake.
Post a Comment