BAADHI ya viongozi wa dini na wananchi
wamesema shutuma za aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa kuwa baadhi yao walihongwa na
Mgombea Urais wa Ukawa kupitia Chadema, Edward Lowassa, ni upuuzi mtupu.
Wamemtaka atoe ushahidi wa madai hayo
kwa kutaja majina ya viongozi na kiasi walichohongwa, wakisisitiza kuwa
hizo ni siasa za majitaka na kwamba anaifanyia kazi CCM ili apate njia
ya kurudi katika chama hicho.
Rais wa TEC azungumza
Rais wa TEC azungumza
Akizungumzia shutuma hizo, Makamu wa
Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Askofu
Severin Niwemugizi, amemtaka Dk. Slaa kutoa ushahidi wa madai yake kuwa
maaskofu wa kanisa hilo wamehongwa na Edward Lowassa.
Akizungumza kwa simu yake ya mkononi,
Askofu Niwemugizi alieleza kushangazwa na tuhuma hizo zilizotolewa na
Dk. Slaa dhidi ya maaskofu bila uthibitisho.
“Hizo taarifa ndiyo nazisikia kwako, lakini kama kweli amesema hivyo kwa nini hakuweka ushahidi kuanzia majina ya maaskofu hao waliopewa fedha, kiasi na zilikopokelewa. Lakini kwa upande wangu binafsi sijapokea kiasi chochote kutoka kwa mtu yeyote.
“Hizo taarifa ndiyo nazisikia kwako, lakini kama kweli amesema hivyo kwa nini hakuweka ushahidi kuanzia majina ya maaskofu hao waliopewa fedha, kiasi na zilikopokelewa. Lakini kwa upande wangu binafsi sijapokea kiasi chochote kutoka kwa mtu yeyote.
Askofu Niwemugizi alimtaka Dk. Slaa
kutoa uthibitisho wa maaskofu wa kanisa hilo kupokea fedha kutoka kwa
Lowassa waweze kutoa uamuzi.
“Lowassa nimewahi kukutana naye
nilimwalika kwenye shule yangu ya seminari kule Biharamulo… shule
yenyewe inaitwa Katoke na nilimuweka wazi sababu za kumwalika na
sikupokea kiasi chochote cha fedha kutoka kwake,”alisema askofu huyona
kuongeza:
“Athibitishe hilo aonyeshe kiasi cha
fedha na majina ya maaskofu, mimi sijapata kiasi chochote labda kama
nimetupiwa kwenye akaunti yangu bila mimi kujua lakini nasisitiza atoe
ushahidi.”
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Madhehebu ya Dini nchini, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kipentekosti, William Mwamalanga alisema kauli za Dk. Slaa zina dalili ya kuleta kisasi fulani.
Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Madhehebu ya Dini nchini, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kipentekosti, William Mwamalanga alisema kauli za Dk. Slaa zina dalili ya kuleta kisasi fulani.
“Angekuja mapema kabla ya taratibu hizi
kuanza tungemwelewa lakini kwa sasa yupo nyuma ya wakati. Kwanza
ameonekana amesukumwa afanye aliyofanya na hilo haliwezi kuwabadilisha
Watanzania walioamua kutaka mabadiliko,”alisema na kuongeza: “Hotuba
yake haina mashiko na taifa halihitaji watu wabinafsi,”alisema Mchungaji
Mwamalanga.
Askofu Gwajima azungumza
Naye Askofu wa Kanisa la Ufufuo na
Uzima, Josephat Gwajima amekana kuwa mshenga wa Edward Lowassa kujiunga
na Chama cha Demokrasia na Maendelea (Chadema) .
Pia amekana kuhusika kuwarubuni kwa
fedha maaskofu 30 wa Kanisa Katoliki ambao wanadaiwa kumuunga mkono
Lowassa katika mbio zake za urais baada ya kuhongwa fedha.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Askofu
Gwajima alisema Dk. Slaa ndiyo risasi ya mwisho iliyokuwa imebakia ndani
kati ya bunduki ya CCM ili kuwaokoa.
Alisema yote yaliyosemwa na Dk. Slaa ni
tuhuma za uongo hivyo wananchi wazipuuze kwa kuwa mwanasiasa huyo
anatafuta uungwaji mkono kwa wananchi aelekee CCM.
“Yaani ni uongo kabisa tena uongo
mweupe, imedhihirisha wazi kuwa huyu mtu asingefaa kuwa rais. Ni dhahiri
ameona akiwasema wanasiasa wenzake watamjibu kwenye majukwaa yao ya
siasa, lakini sasa amewasema maaskofu kwa kuwa wao hawana majukwaa.
“Kwa hiyo namshauri hayo mambo ya
kuwahusisha maaskofu na uchaguzi aache uongo wa namna hiyo. Nafikiri
awaseme wanasiasa wenzake kuzungumzia mambo ya siasa ila kuwahusisha
maaskofu si mambo ya busara,” alisema.
Akizungumzia suala la kuwa mshenga wa
Lowassa na Chadema, Askofu huyo alisema anafikiri Dk. Slaa ametumwa na
waliomtuma, hivyo anawafanyia kazi watu.
“Kwa kawaida inashangaza kwamba kama
watu wawili wanagombana, inatakiwa awepo mtu wa kuwaunganisha, ila
anaposema maaskofu 34 haileti maana, haiingii akilini… ameingiza
Gwajima, Rostam (Aziz) na maaskofu, haeleweki anachozungumza. Lakini
ninachosema kuna waliomtuma ni watu ambao anawafanyia kazi.
“Kikubwa ni kwamba baada ya Lowasaa
kuchaguliwa kugombea urais kwa Chadema alichukia, alifikiri Lowassa
hataendelea kuwa na umaarufu, sasa anaona Lowassa anakwenda, hiyo
imemtia hasira anataka kumchafulia Lowassa, ndiyo maana anaongelea
Lowassa Lowassa tu.
“Kwa mfano alisema Lowasa angekuja na
wabunge wenyeviti wa CCM, ina maana angemkubali Lowassa aje nao, sasa
angekuja nao asingekuwa fisadi? Ni swali zuri ila amekwepa kulijibu.
“Nafikiri Dk. Slaa ndiyo risasi ya
mwisho iliyobakia ndani ya bunduki ya CCM. Natoa wito kwa waumini wangu
wafahamu kuwa hizi tuhuma ni za uongo na namsihi huyo daktari asihusishe
maaskofu na uongo wake abaki nao mwenyewe,” alisema Askofu Gwajima.
Maoni ya wananchi
Alphonce Boniface ambaye alipiga simu na
kujitambulisha kuwa ni mpiga kura, alisema Dk. Slaa ambaye jana
alijitambulisha kuwa ni mtu masikini na anashindia mihogo, awaeleze
Watanzania fedha alizotumia kuita waandishi wa habari katika hoteli
kubwa ya Serena pamoja na kulipia vipindi vilivyorushwa moja kwa moja
vimegharamiwa na nani.
Alisema alichokisema Dk. Slaa ni
kukipigia debe Chama Cha Mapinduzi (CCM) na anachokitaka ni kuingia
katika kampeni za chama hicho.
“Orodha ya mafisadi aliowataja … ni vema
angeenda kushtaki Serikalini/mahakamani ili Lowassa achukuliwe hatua na
si kuwaeleza wananchi kwani kufanya hivyo hakuna faida yoyote.
“Tunamtaka Dk. Slaa aache siasa za
majitaka aende mahakamani aeleze yale anayoyajua na kutoa ushahidi ili
Lowassa apelekwe mahakamani au achukuliwe hatua.
Alisema zipo nchi mbalimbali kama vile
Sudan, Kenya na Afrika Kusini ambazo wagombea wao walikuwa na tuhuma za
mauaji, ubakaji, kuhodhi ardhi lakini wananchi waliwapenda na kuwapa
uongozi na wanafanya vizuri.
“Wananchi tunatakiwa tuamke na tuwe
makini kuchagua viongozi ambao wataweza kutatua changamoto
zinazotukabili na si kusikiliza siasa za wagombea ambao wanashindwa
kutekeleza ahadi zao.
Post a Comment