Ikiwa ni
siku ya pili toka sheria ya makosa ya mtandaoni ianze kutumika rasmi,
Ben Pol amedai si rahisi watu kuacha tabia za kuchafua au kutukana
wenzao mara moja.
Akizungumza
na Mjengwablog leo, Ben Pol amesema yeye tayari alishaacha na tabia ya
kusoma kile kilichoandikwa na mashabiki wake kwenye mitandao kwa kuamini
wengine wapo kwaajili ya kumkatisha tamaa.
“Watu hawawezi kuacha kuandika vibaya au vizuri,” amesema Ben Pol.
“Pia
naamini yale matusi ya direct yatapungua kwa kiasi kikubwa. Mimi zamani
hata kama sheria haijaanza niliachaga kuangalia vitu ambavyo vinaweza
nikatisha tamaa, zinakuumiza yaani. Kwahiyo tuangalie matokeo ya sheria
labda hali itabadilika,” aliongeza muimbaji huyo wa Sophia.
Post a Comment