Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ASKARI WANYAMA PORI WADAIWA KUWAPIGA WAFUGAJI NGORONGORO


Askari wa wanyamapori wakiwaadhibu raia katika Operesheni Tokomeza
Askari wa wanyamapori wakiwaadhibu raia katika Operesheni Tokomeza
MGOGORO mpya umeibuka Ngorongoro baada ya Askari wa Wanyamapori wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kudaiwa kuwapiga wafugaji wa kata za Endulen na Alaitole wanaoishi pembezoni mwa hifadhi hiyo.

Chanzo cha mgogoro huo kinaelezwa kusababishwa na baadhi ya wafugaji kupeleka mifugo yao eneo la Mash ambalo hutumiwa kunywesha mifugo yao hasa kipindi cha kiangazi, ambapo askari walipowakuta walianza kuwashambulia kwa madai kuwa hawaruhusiwi kufuga mifugo yao katika eneo hilo.
Wafugaji hao wameeleza kuwa katika kipindi hiki cha kiangazi ambacho wanakabiliwa na uhaba wa maji hasa kwa ajili ya mifugo yao na wamekuwa na utaratibu wa kutumia eneo hilo kwa makubaliano ya kila mwaka ila kwa mwaka huu imekua tofauti kwani wamefukuzwa pamoja na kupigwa na askari hao kinyume cha sheria.
Mzee wa mila jamii ya Wamasai, Kadogo Olduati amesema kuwa kwa kipindi kirefu wameishi katika ardhi mseto yenye mchanganyiko wa wanyamapori na mifugo pamoja na binadamu bila kusababisha athari zozote katika kwa mazingira na wanyama.
Olduati ameitaka Mamlaka ya Ngorongoro isiegemee upande wa wanyamapori na kuwasahau wafugaji ambao hutegemea ufugaji kuendesha maisha yao ya kila siku.
Katibu wa Baraza la Wafugaji, James Moringe ameiomba mamlaka ya Ngorongoro na Baraza la wafugaji kwa pamoja kuitisha kikao cha haraka ili kuepusha mgogoro huo ambao unaweza kusababisha uvunjifu wa amani na kuathiri uhifadhi na utalii kwa ujumla.
Mhifadhi wa Ngorongoro hakuweza kupatikana kuzungumzia tikio hilo kwa kuwa simu yake ya mkononi haikupatikana, lakini pia walinzi waliwazuia waandishi kuingia ofisini kwake mpaka watakapopata kibali maalum.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top