Ndugu zangu,
Wasadikika wako katikati ya msimu wao wa Ngoma Kuu. Katika hali ya kustaajabisha, mara hii Wasadikika wameamua kuwa kila mtu acheze ngoma atakavyo, na aimbe atakavyo. Mdundo ajichagulie mwenyewe na wimbo pia.
Wasadikika wako katikati ya msimu wao wa Ngoma Kuu. Katika hali ya kustaajabisha, mara hii Wasadikika wameamua kuwa kila mtu acheze ngoma atakavyo, na aimbe atakavyo. Mdundo ajichagulie mwenyewe na wimbo pia.
Jambo moja ni ukweli, kuwa Wasadikika hawajapata kuwa wakweli kwa nchi yao waliyozaliwa.
Ni kwa vile Wasadikika hawapendi kuujua ukweli wao. Wasadikika wanaongoza duniani kwa kuwa wanafiki kwa nchi yao waliyozaliwa.
Wasadikika ni mahodari sana wa kuukimbia ukweli. Kuvikimbia vivuli vyao.
Hakuna
namna yeyote itakayowasaidia Wasadikika kufanikiwa kusonga mbele
kimaendeleo, bali ni kwa kutambua, kuwa huu ni wakati wa wao kuwa
wakweli kwa nchi yao waliyozaliwa.
Na hakuna wa kuwasaidia kuujua ukweli wao, bali ni wao wenyewe, kwenye nchi yao ya Kusadikika.
Ni Neno Fupi La Usiku.
Maggid,
Dar Es Salaam.
Mji Mashuhuri kwenye Nchi Ya Wasadikika.(P.T)
Ni Neno Fupi La Usiku.
Maggid,
Dar Es Salaam.
Mji Mashuhuri kwenye Nchi Ya Wasadikika.(P.T)
credit: Mjengwa blog
Post a Comment