Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

NANI WA KUTEGUA KITENDAWILI CHA WAMACHINGA JANGWANI?

Baadhi ya wafanyabiashara ndogondogo waliokuwa wameanza kujenga mabanda eneo la Jangwani jijini Dar wakiwa kwenye mabanda yao.

Hiki ni kibao kinachoonesha mpaka wa kufanyia biashara eneo hilo.…
Baadhi ya wafanyabiashara ndogondogo waliokuwa wameanza kujenga mabanda eneo la Jangwani jijini Dar wakiwa kwenye mabanda yao.(P.T)
Hiki ni kibao kinachoonesha mpaka wa kufanyia biashara eneo hilo.
Taswira ya mabanda yaliyojengwa eneo hilo.
Hapa ni kamba zinazoonesha viwanja vya watu kabla ya kuanza kujenga eneo hilo.
Mwenyekiti wa wafanya biashara ndogondogo, Sadati, Salum Shemboko akionesha bango la Halimashauri ya Manispaa ya Ilala linalowaonesha mpaka wao.
NI nani wa kutegua kitendawili cha wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama ‘wamachinga’ juu ya sakata linaloendelea miongoni mwao baina ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) la kuwataka kuondoka eneo la Jangwani walilokuwa wamehamia kwa ajili ya kufanya biashara zao. 
Hali hiyo imekuja baada ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kupitia kwa Mkuu wa Wilaya Ilala, Raymond Mushi, kuwataka wamachinga wa maeneo ya Ilala Boma na Kariakoo waliokuwa wakitandaza biashara zao chini kuwataka kuhamia eneo la Jangwani, jambo ambalo sasa limezua patashika.
Akizungumza na mwandishi wetu, mwenyekiti wa wafanyabiashara ndogondogo wa eneo la Jangwani, Sadati Salum Shemboko, amesema kuwa anashangazwa na kauli ya NEMC kuwazuia kufanya biashara katika maeneo hayo ya Jangwani wakati wapo pale kwa tamko la Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.
Alisema kuwa mpaka sasa wametumia gharama nyingi kwa kujenga vibanda sehemu hiyo na hawaoni watafidiwaje. Alionya kwamba NEMC na Manispaa ya Ilala wasipokaa pamoja, watasababisha matatizo.
(HABARI/PICHA: DENIS MTIMA/GPL)
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top