Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Maalum ya CCM Zanzibar,
akisalimiana na Rais wa Zanzibar, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa
CCM Zanzibar, Dkt. Mohamed Ali Shein, wakati walipowasili kwenye Ukumbi
wa Ofisi za CCM Kisiwandui mjini Zanzibar kwa ajili ya kuhudhuria katika
kikao cha Kamati Maalum ya CCM Zanzibar, ambacho leo kilipitisha jina
la Dkt. Shein kuwania nafasi ya Urais kwa tiketi ya CCM. Picha na OMR
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dkt. Mohamed Ali Shein, akizungumza
na Wajumbe wa Kamati Maalum ya CCM Zanzibar (hawapo pichani) wakati wa
kikao cha Kamati Maalum ya CCM kilichofanyika leo Julai 5, 2015 kwenye
Ukumbi wa Ofisi za CCM Kisiwandui mjini Zanzibar kwa ajili ya kujadili
na kupitisha jina la Mgombea Urais wa Zanziba kwa Tiketi ya CCM.
(katikati) ni Mjumbe wa Kamati hiyo, ambaye aliongoza kikao baada ya
kuteuliwa kuwa Kaimu Mwenyekiti, Dkt.Mohammed Gharib Bilal na Mjumbe,
Balozi Iddi. Picha na OMR
Kiti
cha Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Mohamed Shein, kikiwa wazi
baada ya kukabidhi madaraka kwa wajumbe ili kujadili na kuteua jina la
mgombea Urais wakati wa Kikao Maalum cha CCM, leo. Picha na OMR
Kaimu Mwenyekiti wa CCM, Dkt.Mohammed Gharib Bilal, akiendesha Kikao hicho maalum cha Kamati Maalum, baada ya kuteuliwa na Wajumbe wa Kamati hiyo. Kushoto) ni Balozi Seif Iddi. Picha na OMR
Dkt.Bilal na Balozi Iddi,wakifurahia baada ya Wajumbe kupitisha Jina la mgombea Mjumbe, Dkt.Bilal, akimpongeza Dkt. Shein baada ya jina lake kupitishwa na wajumbe katika Kikao cha Kamati Maalum ili kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 unaotarajia kufanyika mwezi Oktoba. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali. Picha na OMR
Wajumbe walioshiriki katika Kikao hicho
Picha ya pamoja baada ya kikao hicho.
Kaimu Mwenyekiti wa CCM, Dkt.Mohammed Gharib Bilal, akiendesha Kikao hicho maalum cha Kamati Maalum, baada ya kuteuliwa na Wajumbe wa Kamati hiyo. Kushoto) ni Balozi Seif Iddi. Picha na OMR
Dkt.Bilal na Balozi Iddi,wakifurahia baada ya Wajumbe kupitisha Jina la mgombea Mjumbe, Dkt.Bilal, akimpongeza Dkt. Shein baada ya jina lake kupitishwa na wajumbe katika Kikao cha Kamati Maalum ili kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 unaotarajia kufanyika mwezi Oktoba. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali. Picha na OMR
Picha ya pamoja baada ya kikao hicho.
Post a Comment