Naibu
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Rajab Luhwavi akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM
Taifa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete katika uwanja wa ndege wa Dodoma
ambapo aliendesha kikao maalum cha kamati kuu ya CCM kilichojadili na
kupitisha ilani ya CCM 2015-2020.
.Mwenyekiti
wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu mwenyekiti wa CCM
Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar Dr. Mohamed Ali Shein(kushoto),
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Ndugu Philip Mangula,(kulia) na katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana(Watatu kushoto) wakati wa ufunguzi
wa kukao maalum cha kamati kuu ya Halmashauri kuu ya CCM kilichoijadili
ili kuipitisha ilani ya CCM 2015-2020 katika ukumbi wa White House
uliopo makao makuu ya CCM mjini Dodoma leo.
Mwenyekiti
wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiipitia ilani ya Chama Cha
Mapinduzi 2015-2020 wakati wa kikao maalum cha kamati kuu ya Halmashauri
kuu ya CCM(CC) kilichoijadili na kuipitisha ilani hiyo leo jioni.
Baadhi ya
wajumbe wa Kamati kuu ya CCM akiwemo Makamu wa Wapili wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Balozi Sefu Ally Iddi,Spika wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mh.Anna Makinda na wajumbe wengine waliojadili ili
kuipitisha ilani ya CCM 2015-2020 leo katika ukumbi wa White House
uliopo makao makuu ya CCM mjini Dodoma leo.
Post a Comment