Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Zitto Kabwe: Sitaki kulumbana na CHADEMA



Kiongozi wa chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amesema hawezi kulumbana na viongozi wa chama chake cha zamani cha Chadema kwa kuwa anachofanya sasa ni kutafuta wanachama wa chama chake kipya. 
 
Zitto alisema hayo juzi mjini Morogoro wakati wa mkutano wa ziara ya uzinduzi wa chama hicho uliofanyika katika kiwanja cha ndege mjini hapa.
 
Akihutubia huku akishangiliwa na wananchi, Zitto aliwataka kumpima na kumchuja yeye kwa matendo yake na kwamba kwa sasa jitihada zake amezielekeza mikoani kupata wanachama.
 
“Nimekuwa nikisikia maneno maneno mengi kutoka kwa viongozi wangu wa zamani lakini nawaheshimu na sitoweza kuwajibu kwani siasa za chuki kwa sasa zimepitwa na wakati, ninachofanya ni kukijenga chama,”alisema Zitto.
 
Kiongozi huyo alisema Morogoro ni moja ya mkoa unayoifanya nchi kukosa maendeleo kutokana na viwanda vingi kubinafsishwa na hivyo kutokuwa na faida kwa wananchi.
 
“Morogoro ni mkoa wa sita katika kuchangia pato la Taifa na takribani Sh2.2 trilioni zimekuwa zikipatikana kwa ajili ya maendeleo ya watu wa mkoa huo,” alisema Zitto.
 
Mwenyekiti wa chama hicho, Anna Mghwira aliwataka wanawake nchini kuacha kushiriki siasa za vurugu na malumbano hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.
 
Mghwira alisema ni vyema wakaangalia namna gani nchi inakua kiuchumi na watoto na vijana wanapata elimu iliyo bora ambayo itawafanya kufanya kazi kwa uzalendo.
 
Aliwataka wananchi kuwa na taratibu za kuwakumbuka mashujaa wa Taifa hasa kwa mambo mema na mzuri waliyoyafanya wakati wa uhai wao.
 
Mpaka sasa chama hicho cha ACT kimefanya mikutano yake ya uzinduzi katika mikoa ya Ruvuma, Njombe, Iringa na Morogoro na Dodoma .
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top