Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAMUOMBA RAIS KIKWETE KUTOSAINI MUSWADA HUU WA SHERIA


Wasomi na wananchi mbalimbali, wamemuomba  Rais Jakaya Kikwete, kutosaini Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 huku wakieleza kuwa kama utasainiwa watahamasisha wananchi kuupinga kwa kufanya maandamano ya nchi nzima mitaani.
Aidha, wamesema muswada huo ukisainiwa watatumia kama fimbo kukiadhibu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kutokichagua katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba, mwaka huu.
Walisema hayo jijini Dar es Salaam jana wakati wa mdahalo uliowashirikisha wananchi, wanafunzi mbalimbali wa vyuo vikuu na wahadhiri wa vyuo vikuu kujadili athari za Sheria ya Takwimu  ya mwaka 2015 na Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015.
Wakati wa Bunge la 19 lilohitimishwa Aprili Mosi, mwaka huu, miswada hiyo iliwasilishwa na serikali bungeni kwa hati ya dharura na kupitishwa na Bunge na sasa hatua inayofuata utapelekwa kwa Rais kwa ajili ya kuisaini ili iwe sheria ianze kutumika.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Kitilia Mkumbo, akizungumza katika mdahalo huo alisema miswada hiyo kama itasainiwa na Rais na kuwa sheria, itakuwa na athari kubwa kwa wahadhiri na wanafunzi wa vyuo vikuu.
Profesa Mkumbo alisema kwa mfano, Sheria ya Takwimu ikianza kutumika itarudisha nyuma kupata wanafunzi wa PhD kwa sababu masomo yao yanategemea sana kupata takwimu.
Usalama mkubwa kuliko wote ni uhuru wa kupata taarifa, kutokupata taarifa sahihi kuna hatari,” alisema.
Profesa Mkumbo alisema Watanzania wanapenda kulalamika tu vijiweni lakini hawachukui hatua na kwamba katika suala la muswada huu kuna haja kwa wananchi kuandamana mitaani ili Rais asisaini.
Ndigwa Ezekiel, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alieleza wasiwasi wake kama suala hilo likienda kupingwa mahakamani haki itatendeka kwa madai kuwa imeegemea upande wa serikali.
Wachangiaji wengine walisema kama miswada hiyo itasainiwa, hawataipigia kura CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Wakati wa Mkutano wa Bunge, serikali iliwasilisha Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 na kueleza kuwa mtu akatayebainika kusambaza picha za ngono, miili ya watu waliokufa kwa ajali na usambazaji taarifa za siri za serikali, atatozwa faini ya Sh. milioni tano, kifungo kisichopungua miezi sita au vyote kwa pamoja.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top