Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TAARIFA ZAIDI TUKUO LA KUKAMATWA KWA MAGAIDI MOROGORO


Polisi wakimjulia hali mwenzao aliyekatwa na sime shingoni.
HII ndiyo A-Z ya wale watu tisa wanaoshikiliwa na polisi jijini Dar baada ya kukamatwa msikitini wakiwa na milipuko 30, sare za jeshi na bendera nyeusi inayodaiwa kutumiwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabaab. Mmoja kati ya watu hao (wa kumi), Hamad Makweka aliuawa.Watu hao walikamatwa Aprili 14, mwaka huu saa 3:30 usiku katika Kitongoji cha Nyandero Tarafa ya Kidatu wilayani Kilombero, Morogoro wakiwa na silaha hizo ambapo ilidaiwa kuwa, walikuwa wakijiandaa kwenda kufanya uhalifu wa ‘kigaidi’ mahali.
Ilidaiwa watu hao walilala kwenye Msikiti wa Answar Sunna uliopo Kidatu ambao unamilikiwa na Islamic Foundation.
Baada ya kukamatwa, awali walishikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi, Morogoro na baadaye kupelekwa jijini Dar kwa siri ambako mahojiano makali yanaendelea.
Habari kutoka ndani ya jeshi hilo zinasema kuwa, watu hao wanahojiwa ili kujua ukubwa wa mtandao wao, walikuwa wakafanye tukio wapi na nani mdhafili wao mkubwa.“Unajua kwa sasa tatizo ni kwamba, inaonekana wahalifu wakubwa tunaishi nao, zamani tuliamini wanaweza kuingia kutoka nje ya nchi.
Vitu walivyokutwa navyo.
“Wale jamaa walikuwa wakijiandaa kwenda kufanya uhalifu mahali, hilo ni moja lazima waseme. Pia lazima mtandao wao ujulikane. Jeshi la polisi lilifanya kazi yake kwa usahihi ndiyo maana walinaswa kabla ya muda wa kwenda kufanya tukio,” alisema askari mmoja kwa kuomba jina lake lisitumike kwa kuwa si msemaji wa jeshi hilo. Gazeti la Uwazi lilifika kwenye Msikiti wa Suni na kuzungumza na baadhi ya watu. Mtu wa kwanza kuongea naye alikuwa muumini wa msikiti huo, Shani Kinyimbi ambaye alisema:
“Kwa hili lililotokea, mimi nawaomba viongozi wetu wa msikiti huu kuanzia leo mtu asilale ndani na baada ya swala msikiti ufungwe. Hii ni hatari sana, magaidi kugeuza msikiti sehemu ya maficho imeniuma sana msikiti wetu kuchafuliwa.”
Naye kiongozi mmoja wa msikiti huo, Mohamed Menze ambaye ni mweka hazina mkuu alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo alisema:“Tukio hili la kigaidi limeuchafua sana msikiti wetu na dini yetu kwa ujumla. Kiukweli hawa jamaa sisi kama viongozi wa msikiti hatuwajui na wamefika usiku na kukamatwa usiku huohuo.
Gari la polisi likiwa eneo la tukio.
“Hapa msikitini kuna vijana watatu wanalala ambao ni Hafidh Kondo, Rajabu Shomari, Singo na Mustapha Kivale. Kwa mujibu wa vijana hao, juzi (Aprili 14) usiku walifika watu hao wakiwa na mabegi ya kitalii na kuswali ambapo baada ya kuswali waliomba kulala msikitini
“Wakati wakiendelea kuongea na vijana wetu polisi walifika na kuwakamata na baadaye kwenda kwa imamu wetu ambao walimuuliza kama ana taarifa za ugeni huo imamu alikana kuwa na taarifa, polisi waliwakamata watuhumiwa hao na walipopekuliwa kwenye mabegi yao walikutwa na sare za jeshi, bendera, baruti na vitu vingine mbalimbali. Wakati huo mwenzao mmoja alishauawa.”
Diwani wa Kata ya Kidatu, Bryson Mwanzenye alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo alisema:
“Hili ni tukio la kigaidi na kwa sasa kwenye kata yangu hali ni tete, mtu mwenye ndevu nyingi na kipara (Hamad Makweka) ambaye hafahamiki alivamiwa na kupigwa na wananchi wenye hasira hadi kufa.”
Diwani.
Alipotakiwa kueleza alivyomfahamu marehemu Hamad Makweka alisema: “Huyo mtu si mkazi wa kata yangu, anatoka Ruaha lakini mtu anapokufa ndipo mengi yanapoibuka. Inadaiwa huyo marehemu alikuwa ni mwalimu wa kareti ambaye majirani zake wanasema hawakujua kazi yake lakini alikuwa ni mtu wa kusafirisafiri sana.”
Maulidi Aliphonce ambaye ni dereva wa Bajaj ya pili iliyowachukua baadhi ya watu hao kwenda nao msikitini, alisema:
“Mimi niliwachukua watano kati ya wale watu kutoka kituo cha Ruaha. Mwenzangu (Bajaj ya kwanza) aliwachukua watano. Tukiwa tunaenda msikitini, kwa nyuma tulifuatwa na pikipiki mpaka tunafika msikitini.
“Nilipowashusha, ile pikipiki iligeuza na sisi wa Bajaj tukageuza kurudi kituoni kwetu. Lakini mtu mmoja Hamad Makweka aligeuza na mimi licha ya kwamba wakati wa kuwabeba wenzake na yeye alikuwemo lakini alisema anarudi Kidato kwa sababu wenzake watalala msikitini.
Kiongozi wa msikiti.
“Njiani tukakutana na polisi, wakatusimamisha. Wakaanza kumuuliza maswali Hamad, ghafla naye akatoka mbio, polisi mmoja akamkimbiza, Hamad akatoa sime na kumkata shingoni yule askari na kutaka kuendelea kukimbia, lakini polisi mwingine alimpiga risasi ya mguu, akaanguka na kukamtwa.
“Ndipo wananchi wenye hasira kali walipotokea na kumpiga mpaka wakamuua kwa kumchoma moto. Walimpiga kwa sababu alimkata shingo askari kwa kuulizwa maswali kadhaa.” Naye Koplo Nassoro Dabi ambaye ni mchezaji wa zamani wa Timu ya Polisi, Morogoro aliyekatwa shingo kwa sime na marehemu Hamad ambaye kwa sasa amelazwa Zahanati ya Kikosi cha Kutuliza Ghasia, Morogoro alikuwa na haya ya kusema:
“Namshukuru Mungu hadi leo hii napumua. Kwa kweli nilinusa kifo, sikujua kama jamaa alikuwa na sime kiunoni. Wakati namfukuza aliingia kwenye shimo na kuangua, nilipojiandaa kumkamata alitoa sime na kunikata shingoni nikapoteza fahamu baada ya kutoka damu nyingi.
Msikiti uliohusika na tukio hilo.
“Kama ningejua ana sime ningejua namna ya kumwingia. Lakini kwa kweli ilikuwa hali tete pale. Ila wananchi wa kule wana umoja sana.”Siku za hivi karibuni kumeibuka uhalifu wenye kutia shaka hasa kutokana na silaha wanazokuwa nazo wahalifu hao kiasi kwamba, wapo waliobainika kuwa na ushirika na Kundi la Kigaidi la Al Shabaab la nchini Somalia. Mfano ni kijana Rashid Charles Mberesero (21) ambaye alihusishwa na mauaji ya wanafunzi 148 kwenye Chuo Kikuu cha Garissa nchini Kenya mapema mwezi huu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top