Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MSANII FEROOZ ATIWA MBARONI KWA UTAPELI


Mayasa Mariwata na Makongoro Ogin’g
Tena? Kwa mara nyingine staa wa Bongo Fleva, Ferooz Mrisho ametiwa mbaroni kwa utapeli akidaiwa ‘kuchikichia’ fedha za kumpangisha nyumba jamaa aliyejitambulisha kwa jina la Tony Noah kiasi cha zaidi ya Sh. milioni 3.2 kisha kuingia mitini ikielezwa kuwa nyumba hiyo ina mgogoro.
Staa wa Bongo Fleva, Ferooz Mrisho.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika, ilidaiwa kwamba, staa huyo aliyewahi kutamba na Ngoma ya Starehe amekuwa na tabia ya kuwaingiza watu mkenge kwa lengo la kutafuta mpangaji kwenye nyumba hiyo iliyopo Sinza- Mori, Dar ambayo anaishi na ndugu zake.
Kilitiririka kuwa, awali Ferooz alikuwa akitafuta mpangaji wa nyumba hiyo kupitia kwa dalali ndipo Tony akavutiwa na nyumba hiyo na kukubaliana kutoa kodi ya Sh. milioni 3, 250,000 kwa mwaka.Kilidai kwamba Tony alipomlipa Ferooz fedha hiyo, Machi 14, mwaka huu ndipo akaanza kumpiga kalenda ndipo aliamua kulipeleka shauri kwenye chombo cha sheria.
Kutokana na sekeseke hilo, mwanahabari wetu alimtafuta Tony ambaye alisema kuwa, baada ya kukubaliana na Ferooz kumpa fedha hizo na kuona anaanza kumzungusha kuhamia kwenye nyumba hiyo alimwambia waandikishiane kwenye Kituo cha Polisi Kijitonyama, Dar (Mabatini) kuwa atamlipa fedha hizo Aprili 15 lakini Ferooz hakufanya hivyo.
Kutokana na ishu hiyo, hadi gazeti hili linakwenda mtamboni, Ferooz alikuwa ameshikiliwa Mabatini kwa jalada la kesi namba KJN/RB/3898/15 KUJIPATIA FEDHA KWA NJIA YA UDANGANYIFU.Mwaka jana Ferooz alishikiliwa kituoni hapo kwa msala wa kukamatwa na bangi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top