Watu
watano wamejeruhiwa vibaya na kulazwa katika hospitali ya rufaa
Bugando, baada ya kuangukiwa na kifusi cha ukuta wa jengo la biashara la
Ghorofa saba linalojengwa katika eneo la barabara ya nyerere jijini
Mwanza, huku askari wa kikosi cha zimamoto na uokoaji,polisi na mgambo
wa jiji wakiendelea kumtafuta mtu mmoja anayedaiwa kufukiwa ndani ya
shimo lenye urefu wa zaidi ya mita tatu.
Hawa
ni mamia ya wakazi wa jiji la mwanza wakishuhudia kuanguka kwa ukuta wa
jengo la biashara lililopo kitalu namba 6, block ‘U’mtaa wa Nyerere,
linalojengwa na mkandarasi kampuni ya HYSCON ENGINEERING LTD YA Mwanza.
Muda
mfupi baada ya ukuta huo kuanguka na kusababisha majeruhi, kamati ya
ulinzi na usalama ya wilaya ya nyamagana,ikiongozwa na mkuu wa wilaya
hiyo Baraka Konisaga imewasili katika eneo hilo na kutoa agizo kwa
uongozi wa halmashauri ya jiji la Mwanza.
Kisha
Tukapiga shoto, kulia hadi katika hospitali ya rufaa Bugando ili kuona
hali za majeruhi waliolazwa katika idara ya dharura zinavyoendelea,
ambapo Daktari wa zamu katika idara hiyo Dk. Ernest Elisenguo amesema
majeruhi wawili, Benson Daud na Ramadhan Mkumba hali zao haziridhishi.
Taarifa
iliyoripotiwa na ITV muda mfupi uliopita imesema majeruhi wawili kati
ya watano hali zao sio nzuri.picha kwa mujibu wa millardayo.com
Post a Comment