Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

DANNY MRWANDA AMWAGA WINO YANGA

Danny Mrwanda akitia dole gumba fomu za Mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Yanga SC usiku huu na picha za chini anasaini na akifurahia baada ya kusaini
MSHAMBULIAJI Daniel ‘Danny’ Davis Mrwanda amesaini Mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Yanga SC akitokea Polisi ya Morogoro.
Mrwanda aliyewahi kuwika Simba SC amesaini Mkataba huo usiku huu na amesema mashabiki wa Yanga SC watarajie vitu vizuri.
“Hii ni changamoto kwangu, kusaini klabu nyingine kubwa kama Yanga baada ya kucheza Simba SC wakati fulani, maana yake ninatakiwa kudhihirisha kitu,”amesema Mrwanda akizungumza na BIN ZUBEIRY mida hii.
Mrwanda amesema kwamba Simba SC na Azam FC zote zilifanya naye mazungumzo, lakini hawakufikia makubaliano na baada ya Yanga SC kukidhi matakwa yake, anajitoa kuitumikia klabu hiyo.

 

Mrwanda kutua Yanga SC ni kutimia kwa ndoto zake, kwani wakati anachipukia kisoka aliwahi kwenda kufanya majaribio ya kuomba kusajiliwa, lakini hakufanikiwa mwaka 2005 na karudi AFC ya Arusha.

Mrwanda, mwenye umri wa miaka 31 sasa, aliibukia AFC ya mwaka mwaka 2003 ambako alicheza hadi 2006 alipohamia Simba SC alikocheza hadi 2009 alipokwenda Al Tadamon ya Kuwait.

Alirejea Simba SC mwaka 2009 na akacheza hadi 2010 alipokwenda Vietnam kujiunga na Dong Tam Long An ambayo aliichezea kwa msimu mmoja kabla ya kuhamia Hoang Anh Gia Lai aliyochezea hadi mwaka huu alipojiunga na Polisi Morogoro.

Baada ya kusaini Mkataba huo, usiku huu Mrwanda anakwenda kujiunga na wachezaji wenzake katika hoteli ya Landmark, Mbeazi Beach kwa maandalizi ya mechi ya Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top