Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MADIWANI WA CHADEMA WALIOHAMIA CCM,WARUDI CHADEMA TENA


Aliyevaa nguo ya kijani(CCM) ni bwana Zacharia Mfuko diwani wa CHADEMA kata ya Masekelo katika manispaa ya Shinyanga baada ya kuwasili katika mkutano wa Chadema leo jioni,baadaye alivua nguo hizo na kuomba radhi kuwa alikosea njia baada ya kushawishiwa na viongozi wa CCM akiwemo Stephen Masele,Nape Nauye, Habib Mchange na viongozi wengine wengi ndani na nje ya chadema na CCM,na kueleza kuwa ccm hawana lolote badala ya kulaghai watu.

Kulia ni Sebastian Peter diwani wa Ngokolo akiwasili katika eneo la mkutano,leo.Katika hali ya kushangaza baada ya madiwani hao kuwasili kwenye mkutano vurugu za hapa na pale zilitawala takribani dakika 15 lakini baadaye hali ilikuwa shwari baada ya mbunge Kasulumbayi kutoka jimbo la Maswa mashariki kutumia akili na nguvu nyingi kutuliza wanachama wa Chadema waliokuwa na hasira na kutopendezwa na kitendo cha kuwaleta wasaliti wa chama eneo hilo.
 Hali ilikuwa tete,ngumi zikanukia,kulia ni mmoja wa viongozi wa chadema akikabiliana na wanachama wa chadema waliotaka kuleta vurugu uwanjani hapo.

 Madiwani wasaliti kama wanavyoitwa hivi sasa hapa Shinyanga,wakiwa na nguo za CCM wakiwa wamekaa na viongozi wa CHADEMA baada ya kuwasili eneo la mkutano jioni ya leo.

Mkutano huo ni wa aina yake umehudhuriwa na maelfu ya wananchi wa mkoa wa Shinyanga,kila mtu akiwa na lake moyoni.
Diwani Sebastian Peter kulia akinong'ona jambo na mbunge Kasulumbayi.Picha na Kadama Malunde-Malunde1 blog
Hapa ni katika viwaja vya mahakama ya Mwanzo Nguzo nane mjini Shinyanga ambako leo kumefanyika mkutano wa aina yake ambao pengine unaweza kuuita mkutano wa kihistoria,mkutano ambao uliandaliwa na viongozi wa CHADEMA kanda ya ziwa mashariki wakiongozwa na mbunge wa Maswa mashariki Sylivester Kasulumbayi.Katika mkutano huo wale madiwani wa Chadema ambao mwezi Februari mwaka huu,walijiuzulu na kuhamia CCM,Zacharia Mfuko kutoka kata ya Masekelo na Sebastian Peter kata ya Ngokolo,leo wameomba radhi na kurudi CHADEMA.Miongoni mwa sababu walizozitaja kuchangia kuhama kwao CCM ni chama kinachochonganisha vyama walidanganywa kuhamia ACT lakini wamebaini kuwa ACT na CCM hawana tofauti hivyo kuamua kurudi chadema kwani ndiyo chama imara.Walisema waliahidiwa kuwa wahame Chadema waende CCM ili wajiunge na ACT ili waiimarishe lakini wameshindwa kutofautisha ccm na ACT.Ikumbukwe kuwa walihamia CCM wakidai CHADEMA hakifai kinaendekeza ubinafsi,ukabila n.k,ikafikia hatua wakaitwa madiwani mizigo.Picha na Kadama Malunde-Malunde1 blog
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top