Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

JAMAA ANAPIGANA NA CHATU BILA SILAHA PORINI AKIWAZUIA WASILE WANYAMA!


 Ruben Ramirez mwenye miaka 41 ameamua kujitolea kuingia porini huko Florida, Marekani kupambana na nyoka wakubwa ambao walivamia eneo hilo tangu mwaka 2000 na kula wanyama mbalimbali katika maeneo hayo. Ramirez ambaye ni mwenyeji wa eneo hilo ameeleza kuwa wakati anakuwa, yeye na baba yake walikuwa wakienda porini kuangalia wanyama mbalimbali lakini tangu chatu hao walipovamia eneo hilo hawaoni tena wanyama hao na ndio sababu akaamua kuwapunguza. 
Mwanaume huyo hupigana mieleka na chatu hao na kuwashika wakiwa hai kisha kuwakabidhi kwa maafisa wa wanyama pori wanaowatoa katika eneo hilo kwa lengo la kusaidia wanyama kukua.
 
Ramirez anaeleza kuwa tayari ameshang’atwa zaidi ya mara mia au elfu kadhaa na nyoka hao wakati akipapambana nao lakini ameweza kupona kwa kuwa wengi huwa hawana sumu. 
Pamoja na hatari kubwa anayokabiliana nayo, anadai kuwa hufurahia sana kupigana mieleka na nyoka hao.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top