Hapa nchini Chama tawala CCM kimesema kuwa
kitafanya uchunguzi wa kina ili kujiridhisha kabla ya kuchukua hatua
dhidi ya Waziri mkuu wa nchi hiyo Mizengo Pinda iwapo matamshi yake ya
kutangaza nia ya kuwania Urais wa nchi hiyo kwenye uchaguzi mkuu hapo
mwakani uliambatana na vitendo vya kufanya Kampeini.
Awali chama hicho
kiliwahi kuwaonya baadhi ya vigogo kadhaa ambao walionyesha kuanza
kufanya kampeini mapema ambapo sasa kufuatia hatua ya Kigogo huyo ambaye
ni Waziri mkuu aliyeko madarakani inaanza kufungua mwanya katika mbio
za kuelekea Ikulu hapo mwakani.
Erick David Nampesya amezungumza na Katibu wa
Itikadi wa CCM Nape Nnauye ameanza kwa kusema kutangaza nia ya kuwania
Urais siyo kosa kisheria.
Post a Comment