Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki amejiuzuru

 


Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki

***********

Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasia Jiji la Mbeya Lucas Mwampiki amejiuzuru wadhifa huo kuanzia Aprili mwaka huu kutokana na mkanganyiko wa uongozi ndani ya chama hicho.

Mwapiki amesema amechoshwa na marumbano ya mara kwa mara na meza kuu ndani ya chama hicho katika ngazi ya wilaya hivyo kudhoofisha juhudi zake za kukijenga chama hicho.

Aidha Mwampiki amesema viongozi wa chama hicho wamekuwa na marumbano ya mara kwa mara hivyo yeye kama kiongozi hayupo tayari kuona mambo yanavurugika katika chama hicho.

Hata hivyo katika uamuzi aliouchukua Lucas Mwapiki amesema kuwa yeye atabakia kuwa mwanachama wa chama hicho na Diwani wa Kata ya Mwakibete Jijini Mbeya.

Amewataka wanachama wamuelewe hivyo ameona yeye akae pembeni badala ya kuwa na muda mwingi wa kujadili migogoro ambayo haina tija na kuleta mkanganyiko kwa wanachama.


Na Ezekiel Kamanga
Mbeya yetu
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top